Mabadiliko ya Taarifa kwa waombaji waliofanya udanganyifu wa taarifa
Waombaji hawa ni wale waliowasilisha nyaraka za kughushi au za watu wengine ili kuficha utambulisho wao halisi. Udanganyifu huu, ni ule uliofanyika awali katika usajili na utambuzi
Sheria ya Usajili na Utambuzi ya mwaka 1986 na marejeo ya mwaka 2012 na Kanuni zake za mwaka 2014 kifungu Namba (17) (b) kinaeleza kuwa:
Any person who: “knowingly gives false or misleading information to a registration officer;” commits an Offense and once convicted the person is liable to a fine of not less than two hundred thousand shillings and not more than five million shillings or to imprisonment for a term not less than two months and not more than two years”.
Mtu yeyote ambaye: "Kwa kujua anatoa taarifa za uongo au za kupotosha kwa Afisa Usajili; anatenda kosa na mara baada ya kupatikana na hatia mtu anawajibika kwa faini isiyopungua shilingi laki mbili na isiyozidi shilingi milioni tano au kifungo kisichopungua miezi miwili na kisichozidi miaka miwili”
Mwombaji aliyethibitika kufanya udanganyifu, Mamlaka itafanya marekebisho baada ya kuwasilisha nyaraka zifuatazo:
(i) Nakala ya hukumu/decree order,
(ii) Mwenendo wa kesi,
(iii) Nakala ya malipo ya faini kama atakuwa amehukumiwa hivyo,
(iv) Maelezo ya kukamilika kwa kifungo kama alifungwa,
(v) Nyaraka nyingine kama zilivyo ainishwa katika vipengele vilivyotangulia.